Jumapili, 10 Mei 2015

Semina ya Viongozi, Somo lingine hili hapa

ISHI UKIJUA KUWA NI KIONGOZI
Mwl. E. Kyejo
Neno Kuu:Mdo 8:31-Akasema;Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza?
Maandiko ya somo:
Kutoka 18:14-20, 21-23, 24-27.
Kol 3:23-25

1.       UTANGULIZI:
          Kazi ya Mungu kila inapotajwa huthibitisha kuwa kuna kiongozi ambaye anawatangulia wengine.  Neno la Mungu limekuwa njia ya kuonyesha uongozi wa kweli hata katika ya jamii, ambayo watu wake hawamjui Mungu.  Kiongozi siku zote huonesha njia na kusimama katikati ya changamoto za siku kwa siku.  Changamoto katika kuwaongoza watu waliookoka ni kubwa na ngumu zaidi kuliko kuwaongoza watu ambao hawamjui Mungu.  Kila walipo watu wawili au watatu waliokusanyika kwa jina langu mimi nipo  katikati yao.Mt 18:20.  Yesu Kristo ni mwanzilishi wa uongozi.

Kiongozi ni nani?
Ni mtu anayeongoza kikundi cha watu  ili kufikia lengo/nia walilojiwekea.  Ni mtu aliyekabidhiwa kuongoza watu ili wamjue Mungu na kuurithi uzima wa milele.

2.       SIFA ZA KIONGOZI
          1 Tim 3:1-7
Biblia inasema askofu ni mwangalizi na shemasi ni mtumishi wa kanisa.
a)     Usilaumike
b)    Uwe mume/mke mmoja
c)     Uwe na kiasi na Busara-Kol 3 :5,2Tim 1:7
d)    Uwe wa Utaratibu
e)     Uwe mkaribishaji/mkarimu
f)      Uwe unajua kufundisha-1 Tim 4:16
g)     Usiwe mlevi
h)    Si mpiga watu (mgomvi)-2 Tim2:24
i)       Uwe mpole
j)       Si mtu wa kujadiliana (mbishi)
k)    Usiwe mtu wa kupenda fedha
l)       Uweze kusimamia nyumba yako vema
·        1 Sam: 2:12
m)  Uweze kutisha watoto wako katika ustahivu-adabu na utii. Tito 1:6-9. Mf Eli.
n)    Uwe unashuhudiwa mema- 1Tim 5:10;
2 kor 8:21;1 kor 5:12-13
o)    Uwe unatoa sadaka zote zilizoagizwa na Mungu aliyehai
ü Mal 3:10; Mit 3:9; 1 nya 26:26
ü Mwa 7:11;Law 27:30;Hes 18:21-24
ü Kumb 12;6;14:22-29;Neh 13:12
ü Mt 23:23; Lk 18:12; Mal 3:8
3.       WAJIBU WA KIONGOZI
          Ili utimize sifa za kiongozi ni lazima uwe tayari kutimiza wajibu wako wa kila siku, utekeleze maazimio mbali mbali ambayo yanakuwa yameazimiwa.
·        Kuwafahamu unaowaongoza (waamini) Yn 10:2-3;Flp 2:4, 1 Kor 10:24,33
·        Unatakiwa kuwa Mlinzi Yn10:11-12; Neh 4:9; Mdo 5:23; Flp 2:4.
·        Uwe kielelezo-fanya kwa mfano kusema, kutenda na kuwaza. Yn 10:37-38;1 Tim 1:16
·        Uwe na Imani (kuamini). Yn 11:40;1 The 5:8;1 Tim 1:19, 1 Tim 4 :6
·        Uwe na bidii katika mambo yote.  2 The 3:9-10,Mfano Eliya alionesha bidii 1 pet 5:17
·        Uwe na sikio la Rohoni-Omba-Kol 4:2-3
·        Uwe tayari kujifunza ili ulijue neno la Mungu. Kol 3:16
·        Dumisha umoja/Ushirika. Yn 17:21-26;efe 4:3-4

4.       MAJUKUMU YA KIONGOZI:
a.     Mzee wa Kanisa:Hes 11:16-17; 1 Tim 5:17;Tito 1:5;Yak 5:14;Mdo 14:23
·        Kumshauri Mchungaji  kufikia maamuzi ya kulijenga kanisa
·        Kusimamia maono ya Mchungaji
·        Kusimamia utendaji wa kazi ya kanisa
·        Kupokea taarifa toka kwa mashemasi
·        Kumtia moyo Mchungaji katika maeneo yote ya utumishi wake
·        Kuwatembelea washirika na kuwatia moyo wanaopitia changamoto mbali mbali
·        Kumwombea Mchungaji na familia yake.
·        Kufanya huduma ya maombezi

b.      Shemasi: 1 Tim 3:8-13.
·        Kusimamia usafi kanisani
·        Kusimamia taratibu zote za Ibada
·        Kupokea taarifa za washirika walio katika maeneo yao
·        Kutoa taarifa kwa Mzee wa kanda/mzee wa eneo
·        Kuwatembelea washirika walio katika eneo lako
·        Kusimamia ulinzi na usalama wa mali za washirika kanisani
·        Kupokea washirika na wageni katika ibada

c.      Mwalimu wa Cell: Mdo 20:20
·        Kusimamia washirika walio katika eneo lako
·        Kuwatembelea na kufahamu changamoto zao wanazozipitia.
·        Kuwaombea
·        Kuwafundisha kweli yote ya neno la Mungu
·        Kusoma neno na Kupokea mafundisho
·        Kushiriki ibada kwa uaminifu
d.     Kiongozi wa Idara:
·        Kusimamia malengo ya idara unayoiongoza
·        Kusimamia huduma za idara
·        Kusimamia vikao vya idara
·        Kutoa taarifa ya idara yako kwa Mchungaji
·        Kusimamia maombi katika idara
·        Kusimamia maisha ya ushuhuda katika idara
·        Kusimamia kalenda ya mwaka ya idara

4.       HASARA ZA KIONGOZI ASIYEKUWA TAYARI KUTUMIKA
          Kiongozi akiwa hana sifa anasababisha mkwamo wa watu au kikundi kufikia lengo ambalo walikuwa wanalitarajia.
§  Huwa na tabia za kujitenga na viongozi wenzake kwa kila mamuzi yaliyofanyika.
§  Huwa na tabia ya kujitanguliza
§  Huwa na tabia ya kunung’unika kila wakati.Flp 2:3
§  Hukosa Uvumilivu na Upendo
§  Asiposaidiwa anaweza kusababisha maasi katika ya kundi.

5.       FAIDA YA KIONGOZI ALIYEKUWA TAYARI KUTUMIKA:
          Kiongozi mwenye sifa atasababisha kazi ya kikundi kusonga mbele na kufikia lengo lile ambalo wamejiwekea.
o   Huwatia moyo wengine
o   Husimamia mamuzi ya viongozi wenzake
o   Huwatanguliza wengine-Flp 2:4; 1 kor 10:24,33
o   Huwapenda wote
o   Huwainua watu waliofikia kukata tamaa.

6.       HITIMISHO:

Ili uwe kiongozi bora katika eneo unalolitumikia ni lazima ufanye mambo yafuatayo:
v Lazima uwe tayari kumsikiliza Roho Mtakatifu
v Beba mzigo wa kuomba kila siku-1 The 5:17
v Soma Neno-Kol 3:16, 1 Pet 4:7
v Ishi Maisha matakatifu-Kol 3:5-10.
v Watangulize wengine
v Uwe mtu wa toba-Yak 5:16



Maswali na Majibu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni