Jumamosi, 9 Mei 2015

Viongozi 24 kati ya 60 wakahudhuria semina siku ya kwanza

Somo la kwanza likawasilishwa

GLORY CHRISTIAN CENTRE
SEMINA YA VIONGOZI
MAY 8 – 9, 2015
Na J. Samson

Mstari wa kukumbuka: Mdo 8:31
Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.
Kwanini mtu huyu asimhitaji Mungu amwongoze? Anamhitaji mtu mwenzake amwongoze. Haikanushiki, Kiongozi lazima awepo. Kiongozi huyu ni mimi katika nafasi yangu. Na katika nafasi hii yangu, mimi nami ninamhitaji kiongozi, ndiye huyo au hao walio juu yangu

Maandiko ya Somo letu leo: Kut 18 13 Asubuhi yake Musa akaketi ili awapishie hukumu watu; na hao watu wakasimama kumzunguka Musa tangu asubuhi hata jioni.
 14 Mkwewe Musa alipoyaona yote aliyowafanyia watu, akasema, Ni jambo gani hili uwatendealo hao watu? Kwani wewe kuketi hapo peke yako, na watu wote kusimama kwako tangu asubuhi hata jioni?
 15 Musa akamwambia mkwewe, Ni kwa sababu watu hunijilia mimi wapate kumwuliza Mungu; 16 wakiwa na neno, hunijilia; nami naamua kati ya mtu na mwenziwe, nami nawajuvisha amri za Mungu, na sheria zake. 17 Mkwewe Musa akamwambia, Jambo hili ufanyalo si jema. 18 Huna budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia; maana jambo hili ni zito mno kwako; huwezi wewe kulitenda peke yako.
 19 Sikiza sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe kwa ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao;
 20 nawe utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kuifanya.
 21 Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi; 22 nao wawaamue watu hawa sikuzote; kisha, kila neno lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno dogo wataliamua wenyewe; basi kwako wewe mwenyewe utapata nafasi zaidi, nao watauchukua huo mzigo pamoja nawe.
 23 Kwamba utafanya jambo hili, na Mungu akikuagiza hivyo, basi utaweza kusimama wewe, na watu hawa wote nao watakwenda mahali pao kwa amani.
 24 Basi Musa akasikiza neno la mkwewe, akayafanya yote aliyokuwa amemwambia.
 25 Musa akawachagua watu wenye uwezo katika Israeli yote, akawaweka wawe vichwa juu ya watu, wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi. 26 Nao wakawaamua watu sikuzote; mashauri magumu wakamletea Musa, lakini kila neno dogo wakaliamua wenyewe

Kwa mimi kuwa kiongozi, kazi yangu kuu ni kuwaongoza wengine waende mbele - Kut 15:22 Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji (changamoto zenyewe zipo tu).
Mara ulipochaguliwa kwenye hiyo nafasi yako, kuna mahali unapaswa uwafikishe watu unaowaongoza - Kut 32:34 Basi sasa uende ukawaongoze watu hawa mpaka mahali pale ambapo nimekwambia habari zake; tazama, malaika wangu atakutangulia; pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kwa ajili ya dhambi ya

Kwa maombi umepatikana, hata kama ulipigiwa kura ama uliteuliwa - Numbers 27: 15 Musa akanena na Bwana akisema, 16 Bwana, Mungu wa roho za wenye mwili wote, na aweke mtu juu ya mkutano, 17 atakayetoka mbele yao, na kuingia mbele yao; atakayewaongoza watokapo, na kuwaleta ndani; ili mkutano wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji. (Umuhimu wa kiongozi unabainika hapa - usijidharau)

Pamoja na baadhi ya vigezo, watu huchaguliwa kuwa viongozi wa wengine - 1 Nya 15: 19 Hivyo hao waimbaji, Hemani, Asafu, na Ethani, wakaagizwa kupiga matoazi yao ya shaba kwa sauti kuu; 20 na Zekaria, na Yaasieli na Shemiramothi, na Yehieli, na Uni, na Eliabu, na Maaseya, na Benaya, wenye vinanda vya sauti ya Alamothi; 21 na Matithiya, na Elifelehu, na Mikneya, na Obed-edomu, na Yeieli, na Azazia, wenye vinubi vya sauti ya Sheminithi, 22 waongoze. Na Kenania, mkuu wa Walawi, alikuwa juu ya uchukuzi; yeye aliusimamia uchukuzi, kwa sababu alikuwa mstadi. 23 Na Berekia na Elkana walikuwa mabawabu kwa ajili ya sanduku.

Kuwa na kiongozi ni mbinu nyingine muhimu ya kusonga mbele - 1 Nya 19:16 Na Washami walipojiona kuwa wameshindwa mbele ya Israeli, wakapeleka wajumbe, wakawavuta Washami walioko ng'ambo ya Mto, na Shobaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri, akawaongoza.

Njia kutonyooka wakati wote, kiongozi lazima kujipa moyo ni muhimu sana ili kufikia malengo - 2 Nya 25:11 Amazia akapiga moyo konde, akawaongoza watu wake, akaenda mpaka Bonde la Chumvi, akawapiga katika wana wa Seiri watu elfu kumi.

Je, kuna siku umewahi kujitambua kuwa wewe ni kiongozi wa ngazi hiyo uliyoko? Ayu 31:18 Nami nimekuwa ni kiongozi cha mjane tangu tumbo la mamangu

Kiongozi anapoharibika, waongozwao huonewa na chochote - Isa 3:12 Katika habari za watu wangu, watoto ndio wanaowaonea, na wanawake ndio wanaowatawala. Enyi watu wangu, wakuongozao wakukosesha, waiharibu njia ya mapito yako.  Na ikifikia hatua ya kiongozi kuwakosesha watu wa Mungu, Mungu kuanza kulalamika - Isa 9:16 Kwa maana wawaongozao watu hawa ndio wawakoseshao, na hao walioongozwa na watu hao wameangamia.

Waongozwao nao hugundua ubaya wa kiongozi wao - Omb 3:2 Ameniongoza na kuniendesha katika giza Wala si katika nuru. Mungu huweka tangazo - Micah 7:5 Msimwamini rafiki, msimwekee kiongozi tumaini
  
Kiongozi kutopata maelekezo toka kwa Mungu kupitia Neno na Maombi, hushindwa kupambanua - Mat 23:16 Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga. Pia Mat 23:24 Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia.

Kuna utofauti mkubwa sana wa kuongoza kidunia na kuongoza kiroho - Marko 10: 42 Yesu akawaita, akawaambia, Mwajua ya kuwa wale wanaohesabiwa kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.
 43 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu, 44 na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote. 45 Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.

Tunakuwa viongozi wazuri kwa sisi wenyewe kuongozwa kwanza na Roho Mtakatifu - John 16:13 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. Pia tunapewa karama za maongozi - 1Corinthians 12:28 Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha
Kiongozi mzuri huwa mfano kwa kumheshimu kiongozi wa juu yake - Hebrews 13:7 Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao. Hebrews 13:17 Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi. Hebrews 13:24 Wasalimuni wote wenye kuwaongoza, na watakatifu wote; hao walio wa Italia wanawasalimu

Kuna faida nyingi kwa kuwa kiongozi bora - Daniel 12:3 Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele

Ili ufanikiwe kwenye uongozi wako, lazima ushauriane na viongozi wenzako. Usiache kuitisha vikao - 1 Nya 13:1 Kisha Daudi akafanya shauri na maakida wa maelfu, na maakida wa mamia, naam, na kila kiongozi.

Jihoji: Kikao kikiitishwa na huji, unakuwa umeamuaje? Kutokutafuta walau mrejesho wa kikao, ina maana gani kwako? Unadhani udhaifu wa kiongozi wa kiroho unaambatana na ulegevu kiroho? Kuongoza kulalamika wakati huwajibiki katika nafasi yako ni kusemaje? Kutoshiriki semina yoyote, ina tafsiri ipi? Kama watu hawatoshi kukuelekekeza, nani hatimaye unadhani atafaa kusema nawe? Ili ukubaliane na jambo, ni kwa njia ipi nzuri uambiwe? Unadhani kuchaguliwa na watu kuwa kiongozi ina muunganiko wowote na kupewa nafasi ya kuongoza na Mungu?


Kwa leo tunaishia hapa na Mungu awabariki kwa kujitambua kuwa mu viongozi na mkakubali kuanzia sasa kuwa viongozi bora

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni