Usisahau kutaja mahali ulipo (Barabara/mkoa/wilaya/mtaa) na aina ya chombo cha moto husikaukifanikiwa kutaja namba ya chombo hicho ni vyema zaidi
Kampeni: Namba ya simu ya kutuma ujumbe ikiwa dereva anaendesha kasi
Kutokana na wimbi la ajali za barabarani linalosababisha vifo vya mamia ya watu na maelfu kujeruhiwa, wananchi wametakiwa kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama pindi wanapoona kanuni na sheria za barabarani zinakiukwa na madereva wazembe.
Namba iliyotajwa ni 0800 75 75 75 ambayo itapeleka ujumbe utakaofikishwa katika Makao Makuu ya Polisi kisha mawasiliano kufanywa na askari waliopo katika kituo kinachofuata katika barabara linakopita basi hilo ili lisimamishwe. Taarifa za kukamatwa kwa basi husika zitatangazwa moja kwa moja na Radio One na kuoneshwa ITV.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni